Posts

Showing posts from April, 2017

VISAKRAMENTI KATIKA KANISA KATOLIKI

Visakramenti ni nini? Ni alama takatifu ambazo kwa sababu zinafanana na Sakramenti, zinaashiria kupatikana kwa matunda ya kiroho kupitia maombi ya kanisa. Visakramenti huwasaidia watu kupokea tunda la msingi la Sakramenti na mazingira mbalimbali ya maisha hutakaswa. Katika maana nyengine: Visakramenti ni shara takatifu zilizoanzishwa na Kanisa ambazo lengo lake ni kuwaandaa watu kupokea tunda la Sakramenti na kutakatifuza mazingira mbalimbali ya maisha. Mfano wa Visakramenti: Misalaba, Medani, Rozari, Skapulari, Maji ya baraka, Matawi yaliyobarikiwa, Majivu yaliyobarikiwa n.k Visakramenti hufanyikaje? Visakramenti hufanyika kwa njia ya Baraka. Ukiwa na Msalaba, Rozari Skapurari etc ambayo haijabarikiwa ni kazi bure haiweizi kufanya kazi yoyote. Ni baada ya kubarikiwa na Padre ndipo Visakramenti hupata pumzi ya uhai ndani yake. Hivyo twasema ni katika kubarikiwa Visakramenti hufanya hai navyo huweza kutubariki. NB: Kila Mkristo mbatiwa naye alibarikiwa hivyo huitwa &quo

KANISA LINAISHI MAFUNDISHO YAKE – MSAMAHA

Fr. Innocent Bahati Mushi OFMCap Kanisa liko makini juu ya kile ambacho linafundisha. Linajitahidi kadiri iwezekanavyo kutafsiri mafundisho yake kwa matendo. Linafahamu fika kwamba matendo huongea zaidi kuliko maneno matupu. Kanisa kwa lenyewe limekuwa likiomba msamaha kutokana na madhambi na madhaifu ya wanawe. Huu ni utambuzi kwamba Kanisa ni la kimungu lakini pia ni taasisi ya kibinadamu, watu ambao wamejeruhiwa na dhambi ya asili na wana maelekeo ya dhambi. Wakati wa hija, huko nchi takatifu tarehe 23 Marchi, 2000, Papa Yohani Paulo II alienda Yad Vashem, sehemu ya kumbukumbu ya maangamizi ya Waisrael (Holocost). Huko Papa alisema:  “Kama Askofu wa Roma, na Khalifa wa Petro, ninapenda kuwahakikishia Wayahudi wote kwamba Kanisa Katoliki, likisukumwa na nguvu ya ukweli na upendo wa kiinjili, bila kuingiza mambo ya kisiasa ndani yake, linahuzunishwa na kusikitishwa na kitendo cha Wakristo, wa wakati wowote na mahali popote, kuwachukia, kuwatesa na hata kuwaua ndugu Wayahu

AFYA NJEMA – NINI MAANA YAKE? KUELEKEA MSAMAHA

Fr. Innocent Bahati Mushi OFMCap Moja ya jambo ambalo ni kama mwiba katika ngozi ambalo sisi binadamu tunaalikwa kulifanya ni kuwasamehe waovu kwa kuwatendea mema, na kuwasamehe hata yale yanaonekana hayasameheki. Tunapenda kusoma masimulizi ya watu waliofanikiwa kusamehe uovu waliotendewa kwa upendo, lakini hali hiyo inapotusibu sisi wenyewe, kinachoendelea ndani yetu ni hasira, chuki, mfadhaiko, tunaishiwa nguvu kabisa kiasi cha kuchanganyikiwa. Tunatumia nguvu nyingi sana kupambana na uovu ule na kutaka kulipiza kisasi.  AFYA NJEMA – UTAFITI CHUO KIKUU HAVARD Stadi za maisha na tafiti mbalimbali zilizofanywa Havard University  2001 zinaonesha kwamba kama tunataka kuwa na afya njema, kuishi muda mrefu pasipo msongo moyo na mfadhaiko usio na maelezo, ni lazima tujenge utamaduni wa kuachilia maumizo ya zamani na kuwa na mtazamo chanya juu ya wenzetu hata wale wanaoonekana kuwa ni maadui zetu. Katika wema tunashinda mengi, katika ubaya tunaelekea kuzama katika uovu na uadui