Posts

Showing posts from February, 2017

Je, ni sahihi kutumia vyombo vya muziki wakati wa Kwaresma?

Utangulizi Msingi wa swali hili ni kwamba, kipindi cha kwaresma ni kipindi cha ukimya, tafakari na majonzi yanayoambatana na kuyawazawaza mateso, kifo na kisha ufufuko wa Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristu. Katika wakati kama huu je, ni sahihi kutumia vyombo vya muziki ? Jibu Katika Ibada Katika kujibu swali hili nitatumia "General Instruction of the Roman Missal" ambayo unaweaza kuipata  kwa kubonyeza hapa Ukisoma kifungu namba 313 kuhusiana na matumizi ya vyombo vya muziki katika kipindi cha kwaresma inaelezwa kuwa; Vyombo vya muziki vitatumika katika kusaidia uimbaji. Isipokua katika sikukuu na sherehe mfano jumapili ya matawi. Hii ina maana kuwa matumizi ya vifaa vya muziki lazima yawe na lengo moja tu la kusaidia uimbaji. Vifaa kama ngoma, magitaa na vinginevyo vyenye kuonesha hali ya sherehe au tafrija haviruhusiwi katika kipindi hiki, isipokua sikukuu kama ilivyoainishwa. Lakini matumizi ya kinanda (bila ngoma) yanaruhusiwa ili kusaidia uimbaji na tafa

ZINGATIA HAYA UNAPOFUNGA KWARESIMA

Utangulizi Moja kati ya mambo yanayoambatana na kipindi cha Kwaresima ni kufunga. Pamoja na hili pia kuna kusali, kutoa sadaka, kufanya toba na kushiriki matendo ya huruma. Katika kipindi hiki waamini tunaalikwa kufunga kama sehemu ya majuto na toba kutokana na dhambi zetu tulizozitenda. Katika  maana pana kufunga ni moja kati ya njia za kutafuta ukaribu zaidi na Mungu. Kufunga ni kujinyima chakula, maji, vitu au mambo ya kidunia kwa utukufu wa Mungu. Sheria juu ya kufunga Ni Amri ya kanisa kufunga siku ya Jumatano ya majivu na kutokula nyama siku ya Ijumaa kuu. Vivyohivyo katika sheria za kanisa, sheria namba 1250 mpaka 1252 zinaeleza kuwa Ijumaa zote pamoja na kipindi cha kwaresima ni siku za toba. Vijana wa kuanzia umri wa miaka kumi na minne mpaka wazee wa umri wa miaka sitini wana wajibu katika kanisa wa kufunga na kujinyima katika siku hizo za toba. Ungalizi wa kanisa na wazazi unahitajika kuwaeleza watoto maana haswa ya kufunga. Hali kadhalika wazee, wajawazito, wa

IFAHAMU JUMATANO YA MAJIVU

Image
“Rarueni mioyo yenu wala si mavazi yenu....” Yoeli 2:13 UTANGULIZI Jumatano ya majivu ni mwanzo wa kipindi cha kwaresima katika kanisa. Ni ishara ya kuanza kwa siku arobaini za kutafakari kwa undani fumbo kuu la upendo wa Mungu linalofunuliwa kwa kujitoa kwake na kufa msalabani, kifo cha aibu ili kuichukua aibu yetu. Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu. KWA NINI TUNAPAKWA MAJIVU? Majivu ni ishara ya majuto, nayo hufanywa visakramenti kwa kubarikiwa na kanisa. Tunapopakwa majivu katika paji la uso hutusaidia kutafakari na kutukumbusha kuwa wanadamu sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi. Hutukumbusha zaidi kuwa maisha ya hapa duniani tunapita na safari yetu itakamilika pale tutakapoungana na Bwana na mwokozi wetu katika ufalme wako. Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13 KWA NINI MAJIVU YAPAKWE KATIKA PAJI LA USO NA SI PENGINEPO? Ishara yoyote iwekwayo katika p

Tumekosa Kweli (Kwaresma)

Zaeni Matunda Mema (Tafakari)

Siku ya Ubatizo wangu (Tafakari)

Kiapo Cha Ubatizo (Tafakari)

Jenga Urafiki (Tafakari)

Yesu Wangu Niokoe (Kwaresma)

Yesu Akalia kwa Sauti Kuu (Kwaresma)

Mungu Wangu Mbona Umeniacha (Kwaresma)

Mungu Unihifadhi Mimi (Kwaresma)

Laumu Imeuvunja Moyo wangu (Kwaresma)

Kwa nini Wasimama Mbali (Kwaresma)

Ee Bwana Kumbuka (Kwaresma)

Bwana ni Kinga na Ngome Yangu (Kwaresma)

Bwana Ndiwe Mchungaji Wangu (Kwaresma)

Bwana Kama Wewe (Kwaresma)

Pasipo Makosa (Kwaresma)

Nimekukimbilia (Kwaresma)

Mungu Wangu (Kwaresma)

Mtazame Mwokozi (Kwaresma)

Msalabani (Kwaresma)

Mateso yako (Kwaresma)

Kwa Ishara ya Msalaba (kwaresma)

Kristu amekua mtii (kwaresma)

Kristu Alijinyenyekeza (Kwaresma)

Kabila langu (Kwaresma)

Ee Bwana usikie (Kwaresma)

asiregewe moyowe