Posts

Showing posts from March, 2017

IFAHAMU SALA YA BWANA (BABA YETU)

Utangulizi Wanafunzi wa Yesu walimuomba awafundishe kusali kama vile ambavyo Yohana aliwafundisha wanafunzi wake kusali. Naye Bwana akawafundisha sala ambaya inatambulika zaidi kama Sala ya Bwana (kwa sababu Bwana mweyewe ndiye aliyeifundisha) aliwaambia msalipo semeni hivi; "Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea, usitutie katika vishawishi, Lakini utuopoe na yule muovu" Nyongeza katika sala ya Bwana, Baadaye katika sala ya Bwana maneno yafuatayo yaliongezwa "Kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele Amina."  Ukuu wa sala ya Sala ya Bwana Sala hii imepokea heshima na hadhi kubwa kwenye kanisa tangu wakati huo mpaka leo. Mababa wa Kanisa katika mapokeo, mfano Mtakatifu Agoustino anasema; "Zipitieni sala zote zilizo katika maandiko na siamini kama mtakuta humo kitu c

IFAHAMU SAKRAMENTI YA KITUBIO/UPATANISHO

Image
Maana Sakramenti ya kitubio pia huitwa sakramenti ya Upatanisho, ipo katika fungu la sakramenti za uponyaji. Kuna Sakramenti mbili za uponyaji, kitubio na mpako mtakatifu wa wagonjwa. Dhumuni haswa la Sakramenti ya uponyaji ni kuzirejeshea uhai roho zetu pale zinapougua kwa kutenda dhambi. Yesu ndiye tabibu mkuu wa roho zetu naye yu tayari kututibu kila tunapougua. (Katekisimu Katoliki 1420,1421) Sakramenti ya kitubio huhusisha, kutambua makosa, kujuta na kuungama pamoja na kuweka nia ya kutotenda dhambi hiyo tena. Kitubio hutusafisha dhambi tulizozitenda baada ya ubatizo. Tunakumbuka, siku ya ubatizo tulipewa kitambaa cheupe, ikiwa ni ishara ya kuwa sasa tumekuwa wapya. Lakini kadri tunavyosongwa na mambo ya dunia, kitambaa chetu cheupe kinachafuka nacho chahitaji kusafishwa, ndio maana tunapata Sakramenti ya kitubio. Wakati gani unahitaji Sakramenti ya kitubio Kila wakati unapotenda dhambi unahitaji Sakramenti ya kitubio. Usisubiri ukirundika dhambi zako ili

UNGAMA, TUBU KAMA DAUDI (Uchambuzi wa Zaburi ya 51)

Wataalamu wa fasihi wanaeleza kuwa ushairi au utenzi ni namna ambayo binadamu huitumia kueleza hisia zake za ndani kabisa. Ni katika mwangaza huu napenda nikushirikishe utenzi wa Daudi unaopatikana katika Zaburi ya 51. Daudi aliandika utenzi huu baada ya kutenda dhambi kubwa iliyokua chukizo kwa Mungu. Daudi alitumia madaraka yake, kutembea na Bath-sheba mke wa Askari wake (Uria), kisha baada ya hayo Daudi alimuua Uria ili kuificha dhambi yake. Mungu alimtuma Nabii Nathani, aende kwa Daudi kumweleza kuwa amechukizwa na dhambi aliyotenda Daudi. Kwa majuto makuu Daudi alilia mbele ya Bwana Mungu akitubu (2 Saweli 11, 12:1-15) . Zaidi ya hayo aliiandika zaburi hii tuitumiayo sana katika kipindi hiki cha Kwaresima. Uchambuzi wa Zaburi hii ya 51 unalenga kutusaidia kuungama na kutubu katika dhati na unyoofu wa moyo, pia hutupatia mambo ya kuzingatia wakati wa kuungama. Mambo haya nikuelezayo ni muhimu kuyafanya wakati unatafakari, kabla ya kwenda katika kiti

Je wewe ni Simeoni wa Kirene? (Tafakari)

Tunasoma katika Injili ya Mtakatifu Marko 15:21, habari za Simeoni wa Kirene aliyemsaidia Yesu msalaba. Ni mstari mmoja tu, lakini wenye maana kubwa sana katika Imani. Kanisa kwa kutambua mchango wa mstari huu mmoja, umetenga kituo cha tano katika Ibada ya njia ya msalaba, kutafakari fumbo hili kubwa. Nataka nikukaribishe tuutafakari mstari na fumbo hili la Simeoni wa Kirene anayemsaidia Yesu Msalaba. Mazingira ya tukio Simeoni alikua anatoka shambani kuelekea nyumbani kwake. Yamkini hakua anafahamu ni jambo gani linaloendelea wakati ule, au kama alikua anafahamu basi halikua jambo la msingi sana kwake. Maana kama angekua ni mwamini au mwanafunzi wa Yesu Kristo asingekua anatokea shambani wakati ule, lazima angekua katika hali ya huzuni na majonzi. Simeoni yamkini alisogea katika msongamano ule wa safari ya kuelekea Kalivari baada ya kuona mkusanyiko mkubwa wa watu, ni hulka ya binadamu kupenda taarifa. Labda alijongea ili kujua ni nini kinaendelea. Lakini ghafla, anashur

Kwaresima: Jifunze, Tafakari juu ya fumbo la Shamba la Mizabibu (Isaya 5:1-7)

Katika Isaya 5:1-7, Nabii Isaya, anaeleza fumbo fupi kupitia kisa cha shamba la mizabibu. Kisa cha Shamba la Mizabibu? Anaeleza; Mkulima alikua na shamba la mzabibu, mahali pa kilimani penye kuzaa sana, kwa kulijali akalipalilia, akalisafisha, akaweka samadi iliyo nzuri, akalitengenezea na kisima cha maji ndani yake. Akitegemea kuwa litazaa zabibu zilizo njema na safi lakini likazaa zabibu mwitu, zabibu chungu. Kisha anauliza akisema; Je, ni jambo gani nililopaswa kulitenda katika shamba langu la mizabibu na sikulifanya? Mbona nalipotegemea litazaa zabibu safi limezaa zabibu mwitu? Fumbo hili lina maana gani? Mkulima ni Mungu, na shamba la mizabibu ni sisi binadamu kila mmoja kwa nafasi yake. Kazi aliyoifanya mkulima ya kuliandaa shamba la mizabibu ni zawadi, vipawa, na talanta ambazo Mungu ametujalia. Zabibu ni matunda yatokanayo na zawadi, talanta na vipawa ambavyo Mungu ametujalia. Fumbo hili lina uhalisia gani? Katika maisha yetu Mungu ametu